Habari motomoto zilizojili hivi punde kutoka kila kona ya Dunia

Saturday, 17 December 2016

Rodrigo Duterte: Rais wa Ufilipino Ameiambia Marekani Iondoe Wanajeshi Wake Nchini Ufilipino


Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte ameiambia Marekani ijiandae kuondoa wanajeshi wake nchini Ufilipino.


Bwana Duterte amesema huenda akafanyia marekebisho muafaka wa kijeshi uliyofikiwa kati ya mataifa hayo,ambayo inawaruhusu maelfu ya wanajeshi wa Marekani kuwa nchini humo kisheria.
Rais huyo hata hivyo ,amesema uhusianao kati ya mataifa hayo mawili huenda ukaimarika chini ya utawala wa Donald Trump
Habari zaidi zinasema matamshi Duterte huenda yamechangiwa na uamuzi wa Marekani kusitisha msaada wake kwa Ufilipino kufuatia sera yake ya kuwapiga risasi na kuwaua wahalifu wa ulanguzi wa dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment