Habari motomoto zilizojili hivi punde kutoka kila kona ya Dunia

Monday, 26 December 2016

BOMU LA VITA YA PILI YA DUNIA LAWALAZIMU WATU 54,000 KUYAHAMA MAKAZI YAO NCHINI UJERUMANI




Wananchi katika mji wa Augsburg nchini Ujerumani jana walijikuta katika mshituko na mshangao mkubwa, bomu kubwa la vita ya pili ya dunia liligunduliwa katikati ya mji wa Augsburg, zaidi ya nyumba 32, 000 zenye idadi ya watu wapatao 54, 000 walilazimika kuyahama makazi yao ili kujiepusha na madhara makubwa. 

Watu 54, 000 waliondoka katika eneo hilo jana katika asubuhi ya krismasi (Jumapili) kutoka mji wa Augsburg, Ujerumani. Barabara zote zinazopita katika mji huo zimefungwa zote toka jumapili tarehe 25 disemba 2016 kuruhusu wataalamu wa mabomu kulitegua. Bomu hilo lilikuwa limewekwa na taifa la uingereza enzi hizo za vita, lina uzito wa tani 1.8. Polisi walishindwa kukadiria ni kwa muda gani wananchi watatakiwa kuwa nje ya makazi yao. Shule za umma zimefunguliwa kutumika kama makazi kwa wahanga wa eneo hilo.
Mara kwa mara mabomu ya Marekani na Uingereza yamekuwa yakipatikana katika miji mbalimbali ya Ujerumanib lakini kwa mara ya kwanza Ujerumani imeshuhudia idadi kubwa ya watu wakiyakimbia makazi yao tangu vita yenyewe.
Mwaka 2011 bomu jengine lilipatikana katika mji wa Koblenz ambalo lilisababisha watu 45, 000 kuhama kwenye makazi yao. Mataifa mengine ya Ulaya pia mabomu ya vita ya pili ya dunia yamekuwa yakipatikana sana. Mwaka 2015 bomu la kijerumani liligundulika nchini uingereza hali iliyopelekea watu 1,500 kuhama makazi yao. Wakati wa vita ya pili ya duniamji wa Augsburg ulikumbwa na mashambulizi mengi ya mabomu kutoka kwa waingereza na wamarekani

No comments:

Post a Comment