Showing posts with label Siasa. Show all posts
Showing posts with label Siasa. Show all posts
Thursday, 30 November 2017
DIALLO, MECK SADIKI NGOMA NGUMU CCM MWANZA
Kuteuliwa kwa DK. Anthony Diallo na Said Meck Sadiki kugombea uenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mwanza kumezua mjadala miongoni mwa wanachama kuhusu anayefaa kutwaa wadhifa huo sasa.
Bunge Lachukua Maamuzi Magumu Kuhusu Wabunge wa CUF
Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema uamuzi wa Mahakama Kuu hauelezi popote kuwa wabunge 8 wa CUF waliopoteza ubunge warudishwe bungeni.
Tuesday, 28 November 2017
Makamu wa Rais Samia Suluhu, Lowassa kukutana Leo Nchini Kenya
Makamu wa rais Mh Samia Suluhu pamoja na Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa wamewasili nchini Kenya leo katika sherehe za kuapishwa kwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Viongozi wengine wa kiserikali waliohudhuria ni pamoja na waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Suzan Kolimba. Sherehe hizo zinafanyika Leo jijini Nairobi baada ya uchaguzi wa marudio uliofanyika mwishoni mwa mwezi wa Oktoba 2017.
Katika uchaguzi huo wa marudio, rais Kenyatta alipata ushindi wa asilimia 98 ya kura zilizopigwa.
Endelea kutembelea blog yako makini ya mchumi Mgejwa kila sekunde
Thursday, 23 November 2017
Alivyouawa Rais John F. Kenedy wa Marekani
Leokatika historia: Novemba 22, 1963 Rais John F. Kennedy ambaye ni rais wa 35 wa Marekani ameuawa kwa kupigwa risasi
Wednesday, 22 November 2017
Je, Baada ya Mugabe Kujiuzulu Anafuata Zima?
Kimya kirefu cha rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma pamoja na chama chake tawala cha ANC kufuatia kujiuzulu kwa Robert Mugabe kinashangaza.
Kinaonyesha ushawishi wa kisaikolojia aliyokuwa nao kwao na walishangazwa sana na hatua aliyochukua. Kile afisi ya rais Zuma ilichosema ni kwamba hatoweza tena kuelekea nchini Zimbabwe kama alivyokuwa amepanga ili kupatanisha kbal ya rais Mugabe kutangaza kujiuzulu.
Ziara hiyo sasa imeahirishwa hadi tyangazo jingine , taarifa ilisema.Lakini badala yake chma cha upinzani nchini Afrika Kusini DA kilijibu na hivyobasi kuungwa mkono na raia weusi pamoja na wazungu kiliposema:
Huu ni ushindi wa raia wa Zimbabwe ambao wametaabika chini ya uongozi wa Mugabe .Habari ya bwana Mugabe sio geni na kwamba inaendelea katika bara la Afrika.
Mtu aliyekuwa shujaa wa taifa lake , Mugabe alisababisha migawanyiko, ukosefu wa udhabiti na kuharibika kwa uchumi wakati alipobadilika kutoka kuwa mpiganiaji wa uhuru hadi kuwa dikteta.
Hilo sio tu kwa Mugabe bali hata Zanu -PF chama ambacho amekitawala kwa kutumia nguvu kwa kuchukua mamlaka tangu taifa hilo lijipatie Uhuru.
Chama cha ANC kinaonyesha ishara kama zile za Zanu-PF, kimekumbwa na ufisadi mkubwa na ghasia huku pande pinzani zikipigania madaraka katika serikali kwa lengo la kujitajirisha badala ya kuwahudumia wananchi.
Baada ya kuchukua madaraka miaka 23 kutoka kwa wazungu ,ANC sasa kinakabiliwa na changamoto ya kujiimarisha au tishio la kuangamiza uchumi wa Afrika kusini kama Zanu-Pf kilivyofanya kwa miaka 37.
David Kafulila Ajivua Uanachama CHADEMA
Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini (2010-2015 ), Mh David Kafulila amejivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kile
Tuesday, 21 November 2017
Mfahamu Robert Mugabe kwa Ufupi
Mwaka 1980, Bw Mugabe alishinda uchaguzi na kuwa waziri mkuu
Mwaka 1982 aliushutumu upinzani kwa kujaribu kupindua serikali
Maelfu ya watu waliuawa alipolituma jeshi lake lililopata mafunzo Korea Kaskizini, kuwakandamiza maadui zake
Mwaka 1987,alibadilisha katiba ili imruhusu kuwa rais na kuongeza mamlaka yake
Uchumi ulidororeka baada ya mwaka 2000…
Wakati Mugabe aliagiza kunyakua mashamba yaliomilikiwa na watu weupe yaliyokuwa kinara ya uchumi
Mfumuko wa bei ulipelekea sarafu ya taifa kuwa bila thamani na hali nchini humo ikazidi kudororeka
Baada ya uchaguzi wa mwaka 2008, Mugabe alilazimika kugawanya mamlaka na kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai
Japo kulikuwa na ghasia dhidi ya wafuasi wa Bw Tsvangirai katika kampeni za uchaguzi
Ndoa yake na Grace Mugabe ,anayemzidi kwa maika 40, yaweza kuwa iliyomponza
Wengi walikasirishwa na Grace kuandaliwa kuwa mrithi wake.
Jeshi limeonesha kumtaka Emmerson Mnangagwa aliyefutwa kazi kama makamu wa Rais na Mugabe mwezi Novemba
CHANZO: BBC SWAHILI
Hatimaye Simba wa Afrika, Robert Mugabe Ajiuzulu
ROBERT MUGABE AMEJIUZULU RASMI URAIS WA ZIMBABWE. Spika wa bunge la Zimbabwe ametoa tangazo hilo na kusema amepokea barua rasmi ya kujiuzulu kutoka kwa Mugabe.
Robert Mugabe alijiuzulu kuwa rais wa Zimbabwe Jumanne, msemaji wa bunge Jacob Mudenda alitangaza.Hii inaleta pazia chini ya utawala wa miaka 37 wa Mugabe.
Mugabe alikuwa ameondolewa kwa nguvu katika utawala wake wa kidemokrasia uliovunjika ndani ya siku kadhaa baada ya jeshi kuchukua udhibiti
"Mimi Robert Gabriel Mugabe kwa mujibu wa kifungu cha 96 cha katiba ya Zimbabwe nimeamua kujiuzulu ... kwa athari ya haraka," alisema msemaji Mudenda, alipokuwa akisoma barua hiyo. Habari hizo zilipelekwa kwenye kikao maalum cha bunge. Kwa haraka.
Orodha ya Wanachama Kutoka Vyama vya Upinzani waliojiunga CCM Leo
Ni bora kuwa Mwanasiasa kuliko MSHABIKI WA SIASA.
Leo hii,hii ni orodha ya wanachama wapya kutoka vyama vya upinzani Tanzania
1.Prof Kitila Mkumbo
Patrobas Katambi Mwenyekiti Baraza la Vijana CHADEMA ahamia CCM
Mwenyekiti
wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) ngazi ya Taifa, Ndugu Patrobas
Katambi amekihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) leo
hii. Patrobas amehama chama cha demokrasia na maendeleo katika muda mfupi tu mara baada ya aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani katika serikali ya awamu ya nne Florence Masha kuhama chama hicho hicho siku chache zilizopita.
Monday, 20 November 2017
Taarifa ya Kofi Annan juu ya Zimbabwe
Njia pekee ya halali na endelevu ya nje ya mgogoro wa Zimbabwe ni kupitia uchaguzi na uadilifu mwaka 2018.
Mgogoro wa kisiasa nchini Zimbabwe haujawahi kutatuliwa. Ninaamini, hata hivyo, kwamba mgogoro huu unatoa ufunguzi wa kipekee kwa upya wa kidemokrasia kulingana na mapenzi ya wazi ya watu wa Zimbabwe. Wanapaswa kuwa mshirika kamili katika azimio la mgogoro huu mkubwa. Makundi ya shauku ambayo yalisafiri katika mitaa ya miji mikuu ya Zimbabwe mwishoni mwa wiki yalidai uhuru, si tu mabadiliko ya uongozi.
Uchaguzi Mkuu nchini Zimbabwe umepangwa kufanyika mwaka 2018. Wao hutoa fursa ya kihistoria kwa wapiga kura wa Zimbabwe kuchagua viongozi wao kwa namna ambayo inatia uhalali kamili juu ya mgombea aliyeshinda. Lengo hilo muhimu litapatikana tu kwa kulinda uaminifu wa mchakato wa uchaguzi. Hii inahitaji kwamba vyama vyote vya kisiasa na wagombea wanaruhusiwa kupiga kampeni kwa uwazi na kwa uhuru bila ya kutishiwa, kwamba vyombo vya habari vinaruhusiwa kutoa chanjo bila ya upendeleo na wapiga kura wa Zimbabwe wanapewa nguvu na kuhimizwa kupiga kura kwa yeyote anayetaka bila hofu au kupende
Tumeona jinsi nchi nyingine za Afrika zimesumbuliwa sana na vikwazo vurugu wakati wa mabadiliko ya kisiasa. Kwa hiyo ninahimiza uongozi wa Zimbabwe - kisiasa na kijeshi - kukuza na kuwezesha mpito kwa demokrasia ya kweli. Viongozi wote wa nchi wanapaswa kuweka kwanza maslahi ya taifa na kufanya kazi pamoja ili kuhakikisha amani ya maendeleo, maendeleo na ustawi wa Zimbabwe....Kofi Annan, Mwenyekiti wa Foundation ya Kofi Annan
General Chiwenga Ahusishwa na Kumzuia Mugabe Kujiuzulu
Kabla ya Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kuonekana mbele ya wananchi kwa mara yake ya kwanza siku ya Jumapili usiku tangu jeshi lilipochukua udhibiti wa serikali, mmoja wa majenerali
Saturday, 29 April 2017
Uchaguzi wawakilishi wa Chadema EALA Mei 10
BUNGE limetangaza kuwa, uchaguzi
mdogo wa kupata wawakilishi wawili wa nafasi ya ubunge kwa Bunge la Afrika
Mashariki (EALA) kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sasa
utafanyika Mei 10, mwaka huu kwenye ukumbi wa Bunge, mjini hapa.
Thursday, 19 January 2017
Mwenyekiti wa Chadema atupwa jela miezi minane
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) akiwemo Kaimu Mwenyekiti wa Mkoa wa Lindi na Mgombea Ubunge
wa Jimbo la Mtama, Selemani Mathew na Katibu wa Chadema Kijiji cha Nyangamara
‘A’ mjini Lindi, wamehukumiwa kifungo cha miezi minane jela bila ya faini
kutokana kufanya mkutano bila ya kibali cha Jeshi la Polisi katika kijiji hicho
wilayani Lindi.
Sunday, 8 January 2017
MBUNGE AHOJI, KWA NINI ASKARI POLISI HAWAMPIGII SALUTI?
MBUNGE wa Kilombero, Peter
Lijualikali kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amemueleza
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba , kuwa hayupo tayari kutoa
fedha za Mfuko wa Jimbo kuchangia kazi za maendeleo ya Polisi jimboni humo.
Saturday, 7 January 2017
Ninapokubaliana na kutofautiana na Magufuli
AWALI ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa
kutulinda, kutupa uhai na afya njema hadi leo. Yote yamewezekana kwa kuwa
amependa sisi wajoli wake tuwe hai na wenye afya.
Saturday, 24 December 2016
Wednesday, 21 December 2016
BALOZI WA KOREA KUSINI AZURU ILEMELA
Safari ya kuijenga Ilemela mpya inazidi kuchanja mbuga ambapo Siku ya jana Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Mhe Song Geum Young amezuru Manispaa Ilemela na kutembelea Kijiji cha Ihalalo kilichopo kata ya Sangabuye eneo linalotarajiwa kujengwa kijiji cha maendeleo mfano wa Semau Dong nchini Korea
Subscribe to:
Posts (Atom)

















